EPISODE · Jul 1, 2026 · 9 MIN
01 JULAI 2026
from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu · host Anold Kayanda
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina. Ikiwa ni siku chache baada ya maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Watu Wasioona na viziwi inayoadhimishwa tarehe 27 Juni kila mwaka, Rashid Malekela wa Idhaa hii anakupeleka Mashariki ya Kati akimmulika mkazi mwenye ulemavu ambaye anakumbwa na changamoto katikati ya vita.Wakati harakati za uokozi na usaidizi zikiendelea nchini Venezuela baada ya matetemeko mawili makubwa ya ardhi yaliyosababisha vifo vya watu zaidi ya 1700 hadi sasa, leo hii ikiwa ni siku ya saba Emily Camargo akiwa kwenye kituo cha hifadhi kilichoandaliwa na Umoja wa Mataifa jimboni La Guaira anaelezea alivyonusurika akisema, “kila kitu kilichonizunguka kiliporomoka na kunizingira, isipokuwa nilipokuweko. Nashukuru kwa sababu jengo la pembeni yetu halikuanguka. Hakuna kilichonipata. Hapa ndio tunalala, mimi, mume wangu , wifi yangu na mbwa wangu. Binadamu yangu na mpenzi wake hatujui waliko tumewatafuta hadi hospitalini, na kwenye orodha, hakuna dalili.”Jopo Huru la Kimataifa la Kisayansi la Umoja wa Mataifa kuhusu akili mnemba, limetoa ripoti leo inayoonesha kuwa teknolojia hiyo inaendelea kusonga mbele kwa kasi kubwa zaidi kuliko uwezo wa serikali kuandaa sera na kanuni zinazoendana nayo. Miaka michache iliyopita, akili mnemba ilikuwa ikitumika zaidi kujibu maswali au kuandika maandishi rahisi. Leo, teknolojia hii inaweza kutengeneza picha na video zenye uhalisia mkubwa na hata kufanya baadhi ya kazi bila usimamizi wa karibu wa binadamu lakini mifumo ya udhibiti na sheria za usalama haijafanikiwa kuendana na mabadiliko hayo.Baada ya miongo kadhaa hatimaye hii leo Umoja wa Mataifa umeondoa kanuni ya kifedha iliyokuwa ikiulazimisha kurejesha kwa nchi wanachama fedha ambazo hazikutumika hata kama fedha hizo hazikuwa zimewasilishwa kabisa. Uamuzi huo uliofanywa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa siku ya Jumanne unafuatia mapendekezo ya Kamati ya Tano, ya Baraza hilo ambayo inashughulikia masuala ya utawala na bajeti. Kanuni ilikwamisha ajira ndani ya Umoja wa Mataifa na operesheni za ulinzi wa amani. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, amesema kuwa kanuni hiyo ilikuwa inahatarisha uthabiti wa Umoja wa Mataifa na kwa uamuzi huu, Baraza limeanzisha mbinu mpya itakayohakikisha kuwa fedha ambazo hazijatumika zinarejeshwa kwa nchi wanachama pale tu zinapokuwa zimewasilishwa taslimu na kupokelewa.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "MKUNGURU."Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
What this episode covers
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina. Ikiwa ni siku chache baada ya maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Watu Wasioona na viziwi inayoadhimishwa tarehe 27 Juni kila mwaka, Rashid Malekela wa Idhaa hii anakupeleka Mashariki ya Kati akimmulika mkazi mwenye ulemavu ambaye anakumbwa na changamoto katikati ya vita.Wakati harakati za uokozi na usaidizi zikiendelea nchini Venezuela baada ya matetemeko mawili makubwa ya ardhi yaliyosababisha vifo vya watu zaidi ya 1700 hadi sasa, leo hii ikiwa ni siku ya saba Emily Camargo akiwa kwenye kituo cha hifadhi kilichoandaliwa na Umoja wa Mataifa jimboni La Guaira anaelezea alivyonusurika akisema, “kila kitu kilichonizunguka kiliporomoka na kunizingira, isipokuwa nilipokuweko. Nashukuru kwa sababu jengo la pembeni yetu halikuanguka. Hakuna kilichonipata. Hapa ndio tunalala, mimi, mume wangu , wifi yangu na mbwa wangu. Binadamu yangu na mpenzi wake hatujui waliko tumewatafuta hadi hospitalini, na kwenye orodha, hakuna dalili.”Jopo Huru la Kimataifa la Kisayansi la Umoja wa Mataifa kuhusu akili mnemba, limetoa ripoti leo inayoonesha kuwa teknolojia hiyo inaendelea kusonga mbele kwa kasi kubwa zaidi kuliko uwezo wa serikali kuandaa sera na kanuni zinazoendana nayo. Miaka michache iliyopita, akili mnemba ilikuwa ikitumika zaidi kujibu maswali au kuandika maandishi rahisi. Leo, teknolojia hii inaweza kutengeneza picha na video zenye uhalisia mkubwa na hata kufanya baadhi ya kazi bila usimamizi wa karibu wa binadamu lakini mifumo ya udhibiti na sheria za usalama haijafanikiwa kuendana na mabadiliko hayo.Baada ya miongo kadhaa hatimaye hii leo Umoja wa Mataifa umeondoa kanuni ya kifedha iliyokuwa ikiulazimisha kurejesha kwa nchi wanachama fedha ambazo hazikutumika hata kama fedha hizo hazikuwa zimewasilishwa kabisa. Uamuzi huo uliofanywa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa siku ya Jumanne unafuatia mapendekezo ya Kamati ya Tano, ya Baraza hilo ambayo inashughulikia masuala ya utawala na bajeti. Kanuni ilikwamisha ajira ndani ya Umoja wa Mataifa na operesheni za ulinzi wa amani. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, amesema kuwa kanuni hiyo ilikuwa inahatarisha uthabiti wa Umoja wa Mataifa na kwa uamuzi huu, Baraza limeanzisha mbinu mpya itakayohakikisha kuwa fedha ambazo hazijatumika zinarejeshwa kwa nchi wanachama pale tu zinapokuwa zimewasilishwa taslimu na kupokelewa.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "MKUNGURU."Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
NOW PLAYING
01 JULAI 2026
No transcript for this episode yet
Similar Episodes
No similar episodes found.