EPISODE · Jul 2, 2026 · 9 MIN
02 JULAI 2026
from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu · host Anold Kayanda
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina tunaangazia fursa ya kufanya mafunzo kwa vitendo au kwa lugha ya kiingereza Internship hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa. Rashid Malekela kutoka Mwanza Tanzania, ambaye aliomba na kupata fursa hiyo anazungumzia na Leah Mushi wa Idhaa hii kueleza ni nini faida yake.Mashirika ya misaada nchini Ukraine leo Alhamisi Julai 2 yameongeza juhudi za kutoa msaada kufuatia ongezeko kubwa la mashambulizi makubwa yaliyofanywa na Urusi usiku wa jana, yakiwemo yale yaliyolenga mji mkuu wa Ukraine, Kyiv na kuwa miongoni mwa mashambulizi makubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa dhidi ya mji huo.Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu ubaguzi wa zama za sasa Ashwini K.P ameonya kuwa ubaguzi wa rangi, chuki dhidi ya wageni, ubaguzi dhidi ya jamii za pembezoni, na aina nyingine za kutovumiliana zinazohusiana na misingi hiyo bado vimejikita kwa kina katika ngazi zote za michezo duniani. Kwenye ripoti yake kwa Baraza la Umoja wa Mataifa la haki za Binadamu, mtaalamu amesema michezo ina uwezo wa kukuza ujumuishi, usawa na mshikamano wa kijamii, lakini bado inaendelea kuakisi na kuendeleza mifumo ya ubaguzi wa rangi na kimaeneo unaoshuhudiwa katika jamii kwa ujumla.Na huko Mwanza, kaskazini-magharibi mwa Tanzania kumeanza mdahalo wa siku mbili wa vijana na amani ulioandaliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP na mmoja wa washiriki anatoa maoni.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
What this episode covers
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina tunaangazia fursa ya kufanya mafunzo kwa vitendo au kwa lugha ya kiingereza Internship hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa. Rashid Malekela kutoka Mwanza Tanzania, ambaye aliomba na kupata fursa hiyo anazungumzia na Leah Mushi wa Idhaa hii kueleza ni nini faida yake.Mashirika ya misaada nchini Ukraine leo Alhamisi Julai 2 yameongeza juhudi za kutoa msaada kufuatia ongezeko kubwa la mashambulizi makubwa yaliyofanywa na Urusi usiku wa jana, yakiwemo yale yaliyolenga mji mkuu wa Ukraine, Kyiv na kuwa miongoni mwa mashambulizi makubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa dhidi ya mji huo.Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu ubaguzi wa zama za sasa Ashwini K.P ameonya kuwa ubaguzi wa rangi, chuki dhidi ya wageni, ubaguzi dhidi ya jamii za pembezoni, na aina nyingine za kutovumiliana zinazohusiana na misingi hiyo bado vimejikita kwa kina katika ngazi zote za michezo duniani. Kwenye ripoti yake kwa Baraza la Umoja wa Mataifa la haki za Binadamu, mtaalamu amesema michezo ina uwezo wa kukuza ujumuishi, usawa na mshikamano wa kijamii, lakini bado inaendelea kuakisi na kuendeleza mifumo ya ubaguzi wa rangi na kimaeneo unaoshuhudiwa katika jamii kwa ujumla.Na huko Mwanza, kaskazini-magharibi mwa Tanzania kumeanza mdahalo wa siku mbili wa vijana na amani ulioandaliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP na mmoja wa washiriki anatoa maoni.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
NOW PLAYING
02 JULAI 2026
No transcript for this episode yet
Similar Episodes
No similar episodes found.