EPISODE · Apr 8, 2026 · 11 MIN
08 APRILI 2026
from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu · host Rashid Malekela
Jaridani tunaangazia sitisho la mapigano nchini Iran, hali ya afya katika ukanda wa Gaza, na elimu kwa watoto walioathiriwa na vita nchini Sudan.Umoja wa Mataifa umekaribisha tangazo la Marekani na Iran la kusitisha mapigano kwa wiki mbili, wakati huu ambapo vita hiyo iliyoanzishwa na Marekani na Israeli dhidi ya Iran ikiingia siku ya 40. Kwa upande wa Lebanon hali bado ni tete kwani Israel inaendelea na mashambulizi katika mji wa Beirut.Madaktari na wahudumu wa afya katika ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel wanaonya kuwa mfumo wa afya katika eneo hilo sasa uko karibu zaidi kuporomoka kuliko wakati mwingine wowote, huku idadi ya wagonjwa ikiendelea kuongezeka, magonjwa ya ngozi na ya kupumua yakienea, na uwezo wa kuwahudumia watu wenye magonjwa sugu ukiendelea kupungua.Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF kwa kushirikiana na Benki ya Dunia linaendelea kurejesha matumaini ya elimu kwa maelfu ya watoto katika Jimbo la Mto Nile nchini Sudan kupitia Programu za Elimu Mbadala (ALP), baada ya miaka mingi ya vurugu na kusitishwa kwa masomo kuathiri mustakabali wao.Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
What this episode covers
Jaridani tunaangazia sitisho la mapigano nchini Iran, hali ya afya katika ukanda wa Gaza, na elimu kwa watoto walioathiriwa na vita nchini Sudan.Umoja wa Mataifa umekaribisha tangazo la Marekani na Iran la kusitisha mapigano kwa wiki mbili, wakati huu ambapo vita hiyo iliyoanzishwa na Marekani na Israeli dhidi ya Iran ikiingia siku ya 40. Kwa upande wa Lebanon hali bado ni tete kwani Israel inaendelea na mashambulizi katika mji wa Beirut.Madaktari na wahudumu wa afya katika ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel wanaonya kuwa mfumo wa afya katika eneo hilo sasa uko karibu zaidi kuporomoka kuliko wakati mwingine wowote, huku idadi ya wagonjwa ikiendelea kuongezeka, magonjwa ya ngozi na ya kupumua yakienea, na uwezo wa kuwahudumia watu wenye magonjwa sugu ukiendelea kupungua.Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF kwa kushirikiana na Benki ya Dunia linaendelea kurejesha matumaini ya elimu kwa maelfu ya watoto katika Jimbo la Mto Nile nchini Sudan kupitia Programu za Elimu Mbadala (ALP), baada ya miaka mingi ya vurugu na kusitishwa kwa masomo kuathiri mustakabali wao.Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
NOW PLAYING
08 APRILI 2026
No transcript for this episode yet
Similar Episodes
No similar episodes found.