EPISODE · Jun 8, 2026 · 9 MIN
08 JUNI 2026
from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu · host Leah Mushi
Hii leo jaridani tunaangazia ujumbe wa Katibu Mkuu kuhusu siku ya baharí duniani na kumulika ni hatua gani Zanziba zinachukua kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Pia tunakwenda nchini Kenya kufuatilia simulizi ya mchezaji wa raga.Bahari duniani zinakabiliwa na changamoto kubwa zinazotishia afya ya mazingira na ustawi wa binadamu, ameonya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres na kutoa wito wa hatua za haraka na za pamoja kukabiliana na hali hiyo.Jamii katika mkoa wa Kaskazini Unguja huko visiwani Zanzibar nchini Tanzania wanaadhimisha siku ya bahari hii leo Umoja wa Mataifa ukielezea dhahiri mafanikio ya mradi wa uhifadhi wa mikoko na ufugaji wa nyuki unaochagiza sio tu upatikanaji endelevu wa kipato bali pia uhifadhi wa mazingira na bahari.Nyota wa mchezo wa raga ama rugby, Kevin Wekesa kutoka nchini Kenya ambaye alishiriki Michezo ya Olimpiki jijini Paris Ufaransa mwaka 2024, ameeleza nia yake ya kufanya vizuri uwanjani huku akitumia umaarufu wake kuhifadhi mazingira na kuhamasisha hatua endelevu kupitia michezo ili kujenga dunia yenye mnepo.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
What this episode covers
Hii leo jaridani tunaangazia ujumbe wa Katibu Mkuu kuhusu siku ya baharí duniani na kumulika ni hatua gani Zanziba zinachukua kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Pia tunakwenda nchini Kenya kufuatilia simulizi ya mchezaji wa raga.Bahari duniani zinakabiliwa na changamoto kubwa zinazotishia afya ya mazingira na ustawi wa binadamu, ameonya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres na kutoa wito wa hatua za haraka na za pamoja kukabiliana na hali hiyo.Jamii katika mkoa wa Kaskazini Unguja huko visiwani Zanzibar nchini Tanzania wanaadhimisha siku ya bahari hii leo Umoja wa Mataifa ukielezea dhahiri mafanikio ya mradi wa uhifadhi wa mikoko na ufugaji wa nyuki unaochagiza sio tu upatikanaji endelevu wa kipato bali pia uhifadhi wa mazingira na bahari.Nyota wa mchezo wa raga ama rugby, Kevin Wekesa kutoka nchini Kenya ambaye alishiriki Michezo ya Olimpiki jijini Paris Ufaransa mwaka 2024, ameeleza nia yake ya kufanya vizuri uwanjani huku akitumia umaarufu wake kuhifadhi mazingira na kuhamasisha hatua endelevu kupitia michezo ili kujenga dunia yenye mnepo.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
NOW PLAYING
08 JUNI 2026
No transcript for this episode yet
Similar Episodes
No similar episodes found.