EPISODE · Jun 10, 2026 · 10 MIN
10 JUNI 2026
from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu · host Flora Nducha
Jaridani leo tunakuletea mada kwa kina maalum ambayo kama nilivyokujuza hapo awali inaangazia mkutano wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu CRPD, unaofanyika hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa chini ya kauli mbiu “kuadhimisha miaka 20 ya mkataba huo na kuimarisha utekelezaji wake katika dunia inayobadilika.”Washiriki wanajadili namna ya kutokomeza ukandamizaji, ukatili na manyanyaso dhidi ya watu wenye ulemavu, kuimarisha mifumo ya huduma na msaada, pamoja na kuongeza ushiriki na uwakilishi wao katika maisha ya kisiasa na umma. Miongoni mwa wanaohudhuria mkutano huo ni Nassriya Nassir Ali mbunge wa watu wenye ulemavu kutoka nchini Tanzania, yeye anaulemavu wa kusikia au kiziwi. Leah Mushi amefanya mahojiano naye na hapa mkalimani wake wa lugha ya Alama Tusajigwe Ernest anajibu kwa sauti. Pia tunakuletea mhtasari wa habari tukimulika haki za elimu kwa watoto nchini Sudan, usalama wa mabaharia na judhibiti wa kusambaa kwa virusi vya Ebola hasa wakati huu wa michezo ya kimataifa ya kuwania kombe la dunia. Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
What this episode covers
Jaridani leo tunakuletea mada kwa kina maalum ambayo kama nilivyokujuza hapo awali inaangazia mkutano wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu CRPD, unaofanyika hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa chini ya kauli mbiu “kuadhimisha miaka 20 ya mkataba huo na kuimarisha utekelezaji wake katika dunia inayobadilika.”Washiriki wanajadili namna ya kutokomeza ukandamizaji, ukatili na manyanyaso dhidi ya watu wenye ulemavu, kuimarisha mifumo ya huduma na msaada, pamoja na kuongeza ushiriki na uwakilishi wao katika maisha ya kisiasa na umma. Miongoni mwa wanaohudhuria mkutano huo ni Nassriya Nassir Ali mbunge wa watu wenye ulemavu kutoka nchini Tanzania, yeye anaulemavu wa kusikia au kiziwi. Leah Mushi amefanya mahojiano naye na hapa mkalimani wake wa lugha ya Alama Tusajigwe Ernest anajibu kwa sauti. Pia tunakuletea mhtasari wa habari tukimulika haki za elimu kwa watoto nchini Sudan, usalama wa mabaharia na judhibiti wa kusambaa kwa virusi vya Ebola hasa wakati huu wa michezo ya kimataifa ya kuwania kombe la dunia. Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
NOW PLAYING
10 JUNI 2026
No transcript for this episode yet
Similar Episodes
No similar episodes found.