EPISODE · Apr 14, 2026 · 9 MIN
14 APRILI 2026
from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu · host Anold Kayanda
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika Mauaji ya kimbari nchini Rwanda ambapo Waziri wa sheria na ambaye pia ni mwanasheria Mkuu wa nchi hiyo Dkt. Emmanuel Ugirashebuja amezungumza na Idhaa hii na anaeleza siri ya wananchi wa Rwanda kuweza kuishi kwa amani baada ya mauaji hayo.Kama mapigano yataendelea nchini Sudan hadi mwaka 2030, umaskini wa kupindukia unaweza kuongezeka na kuvuka asilimia 60, huku watu wengine milioni 34 wakitumbukia kwenye ufukara, imesema Ripoti ya uchambuzi mpya wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) iliyotolewa leo Sudan na Marekani ikiwa kesho inatimia miaka mitatu kamili tangu kuanza kwa vita.Nayo mashirika ya Umoja wa Mataifa yametoa kauli zao tofauti tofauti kuhusu miaka mitatu ya vita nchini Sudan ambapo lile la kuhudumia watoto UNICEF linasema watoto wanaendelea kulipa gharama ya vita kwani zaidi ya watoto 245 wameuawa au kujeruhiwa nchini humo tangu Januari hadi Machi mwaka huu, huku mashambulizi ya ndege zisizo na rubani au droni yamesababisha takriban asilimia 80 ya majeruhi na vifo hivyo.Mzozo wa Israeli na Lebanon ulioshika kasi baada ya wapiganaji wa Hezbollah kushambulia Israeli kupinga hatua ya Marekani na Israeli kushambulia Iran, hii leo huko Washington DC, hapa Marekani kunafanyika mazungumzo kati ya Israel na Lebanon. Umoja wa Mataifa unasihi pande zote kutumia diplomasia kumaliza uhasama na kusongesha azimio namba 1701 la Baraza la Usalama linalozuia mapigano mpakani mwa mataifa hayo mawili.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "KUDA"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
What this episode covers
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika Mauaji ya kimbari nchini Rwanda ambapo Waziri wa sheria na ambaye pia ni mwanasheria Mkuu wa nchi hiyo Dkt. Emmanuel Ugirashebuja amezungumza na Idhaa hii na anaeleza siri ya wananchi wa Rwanda kuweza kuishi kwa amani baada ya mauaji hayo.Kama mapigano yataendelea nchini Sudan hadi mwaka 2030, umaskini wa kupindukia unaweza kuongezeka na kuvuka asilimia 60, huku watu wengine milioni 34 wakitumbukia kwenye ufukara, imesema Ripoti ya uchambuzi mpya wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) iliyotolewa leo Sudan na Marekani ikiwa kesho inatimia miaka mitatu kamili tangu kuanza kwa vita.Nayo mashirika ya Umoja wa Mataifa yametoa kauli zao tofauti tofauti kuhusu miaka mitatu ya vita nchini Sudan ambapo lile la kuhudumia watoto UNICEF linasema watoto wanaendelea kulipa gharama ya vita kwani zaidi ya watoto 245 wameuawa au kujeruhiwa nchini humo tangu Januari hadi Machi mwaka huu, huku mashambulizi ya ndege zisizo na rubani au droni yamesababisha takriban asilimia 80 ya majeruhi na vifo hivyo.Mzozo wa Israeli na Lebanon ulioshika kasi baada ya wapiganaji wa Hezbollah kushambulia Israeli kupinga hatua ya Marekani na Israeli kushambulia Iran, hii leo huko Washington DC, hapa Marekani kunafanyika mazungumzo kati ya Israel na Lebanon. Umoja wa Mataifa unasihi pande zote kutumia diplomasia kumaliza uhasama na kusongesha azimio namba 1701 la Baraza la Usalama linalozuia mapigano mpakani mwa mataifa hayo mawili.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "KUDA"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
NOW PLAYING
14 APRILI 2026
No transcript for this episode yet
Similar Episodes
No similar episodes found.