EPISODE · Jun 15, 2026 · 9 MIN
15 JUNI 2026
from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu · host Anold Kayanda
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kufuatilia ziara ya kihistoria ya Rais wa Baraza Kuu la UN, Annalena Baerbock, kwenye kituo cha kukusanya, kuchakata na kurejeleza taka cha Korogocho (Korogocho Material Recovery Facility - MRF) kujionea namna vijana wanavyogeuza taka kuwa fursa ya kiuchumi na silaha ya kutokomeza umasikini na uhalifu mitaani.Kufuatia makubaliano ya sitisho la mapigano la kudumu baina ya Marekani na Iran yaliyotangazwa jana jumapili Juni 14, viongozi wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa wampongeza kufikiwa kwa makubaliano hayo huku wakihimiza yaheshimiwe na pia kufunguliwe upenyo maalum wa kupitisha misaada ya kibinadamu katika mlango bahari wa Hormuz huko nchini Iran.Kutoka Mashariki ya Kati twende Afrika, ambako mapigano nchini Sudan yanaelezwa kutoonesha dalili yoyote ya kupungua, huku pande zinazohasimiana zikituhumiwa kutumia mbinu za kukamatwa kiholela, mateso na kutoweshwa kwa raia kwa nguvu. Taarifa iliyotolewa leo na Tume Huru ya Umoja wa Mataifa ya Kuchunguza Ukweli kuhusu Sudan imesema vitendo hivyo vinaweza kuhesabiwa kuwa uhalifu dhidi ya ubinadamu.Na leo ni Siku ya siku ya Uelimishaji Kuhusu Ukatili dhidi ya Wazee Duniani ambapo Umoja wa Mataifa umesema hatua zaidi zinahitajika kuwalinda wazee dhidi ya ukatili, huku ukionya kuwa uelimishaji pekee hautoshi na kwamba dunia inapaswa kuimarisha sheria, huduma za afya na mifumo ya kuripoti matukio ya unyanyasaji.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
What this episode covers
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kufuatilia ziara ya kihistoria ya Rais wa Baraza Kuu la UN, Annalena Baerbock, kwenye kituo cha kukusanya, kuchakata na kurejeleza taka cha Korogocho (Korogocho Material Recovery Facility - MRF) kujionea namna vijana wanavyogeuza taka kuwa fursa ya kiuchumi na silaha ya kutokomeza umasikini na uhalifu mitaani.Kufuatia makubaliano ya sitisho la mapigano la kudumu baina ya Marekani na Iran yaliyotangazwa jana jumapili Juni 14, viongozi wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa wampongeza kufikiwa kwa makubaliano hayo huku wakihimiza yaheshimiwe na pia kufunguliwe upenyo maalum wa kupitisha misaada ya kibinadamu katika mlango bahari wa Hormuz huko nchini Iran.Kutoka Mashariki ya Kati twende Afrika, ambako mapigano nchini Sudan yanaelezwa kutoonesha dalili yoyote ya kupungua, huku pande zinazohasimiana zikituhumiwa kutumia mbinu za kukamatwa kiholela, mateso na kutoweshwa kwa raia kwa nguvu. Taarifa iliyotolewa leo na Tume Huru ya Umoja wa Mataifa ya Kuchunguza Ukweli kuhusu Sudan imesema vitendo hivyo vinaweza kuhesabiwa kuwa uhalifu dhidi ya ubinadamu.Na leo ni Siku ya siku ya Uelimishaji Kuhusu Ukatili dhidi ya Wazee Duniani ambapo Umoja wa Mataifa umesema hatua zaidi zinahitajika kuwalinda wazee dhidi ya ukatili, huku ukionya kuwa uelimishaji pekee hautoshi na kwamba dunia inapaswa kuimarisha sheria, huduma za afya na mifumo ya kuripoti matukio ya unyanyasaji.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
NOW PLAYING
15 JUNI 2026
No transcript for this episode yet
Similar Episodes
No similar episodes found.