EPISODE · Jun 16, 2026 · 11 MIN
16 JUNI 2026
from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu · host Feissal Kirwa
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoturejesha hapa Makao Makuu ya UN kusikia mahojiano maalum na ya kina baina ya Flora Nducha wa Idhaa hii na Mkuu mpya wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Dawa na Uhalifu UNODC. Pia tunakuletea Muhtasari wa habari.Kumekuwepo na imani kwamba ugonjwa wa Ebola si halisi, hali iliyowafanya baadhi ya wananchi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kuzika wapendwa wao waliokufa kwa Ebola bila kufuata hatua za kujikinga dhidi ya maambukizi. Kutafuta suluhu ya changamoto hiyo, Shirika la Afya Duniani WHO kwa kushirikiana na Shirikisho la Kimataifa la chama cha Msalaba Mwekundu na Hilali Nyekundu, IFRC, wamesikiliza maoni ya jamii kuhusu taratibu za mazishi.Takriban nusu ya watoto wote duniani au watoto bilioni 1.1 sasa wanakabiliwa na angalau hatari tatu za mabadiliko ya tabianchi zinazolingana, zikihatarisha afya zao, elimu, na maisha yao, imesema ripoti iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF.Na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, yuko nchini Haiti kwa ziara maalum ya mshikamano ili kujionea hali halisi ya wananchi walioathiriwa na ghasia na ukosefu wa usalama. Akiwa huko, Guterres anakutana na wananchi, kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Haiti, na kutathmini juhudi za serikali, Umoja wa Mataifa na jumuiya ya kimataifa za kurejesha utulivu nchini humo.Mwenyeji wako ni Feissal Kirwa, karibu!
What this episode covers
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoturejesha hapa Makao Makuu ya UN kusikia mahojiano maalum na ya kina baina ya Flora Nducha wa Idhaa hii na Mkuu mpya wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Dawa na Uhalifu UNODC. Pia tunakuletea Muhtasari wa habari.Kumekuwepo na imani kwamba ugonjwa wa Ebola si halisi, hali iliyowafanya baadhi ya wananchi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kuzika wapendwa wao waliokufa kwa Ebola bila kufuata hatua za kujikinga dhidi ya maambukizi. Kutafuta suluhu ya changamoto hiyo, Shirika la Afya Duniani WHO kwa kushirikiana na Shirikisho la Kimataifa la chama cha Msalaba Mwekundu na Hilali Nyekundu, IFRC, wamesikiliza maoni ya jamii kuhusu taratibu za mazishi.Takriban nusu ya watoto wote duniani au watoto bilioni 1.1 sasa wanakabiliwa na angalau hatari tatu za mabadiliko ya tabianchi zinazolingana, zikihatarisha afya zao, elimu, na maisha yao, imesema ripoti iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF.Na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, yuko nchini Haiti kwa ziara maalum ya mshikamano ili kujionea hali halisi ya wananchi walioathiriwa na ghasia na ukosefu wa usalama. Akiwa huko, Guterres anakutana na wananchi, kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Haiti, na kutathmini juhudi za serikali, Umoja wa Mataifa na jumuiya ya kimataifa za kurejesha utulivu nchini humo.Mwenyeji wako ni Feissal Kirwa, karibu!
NOW PLAYING
16 JUNI 2026
No transcript for this episode yet
Similar Episodes
No similar episodes found.