PodParley PodParley

17 APRILI 2026

An episode of the Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu podcast, hosted by Leah Mushi, titled "17 APRILI 2026" was published on April 17, 2026 and runs 9 minutes.

April 17, 2026 ·9m · Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

0:00 / 0:00

Hii leo jaridani tunaangazia ripoti ya mauaji wa wanawake na wasichana Gaza, ukatili wa kijinsia na wa kingono unaotumiwa kama silaha ya vita Sudan, na msaada wa dawa na matibabu ya bure nchini DRC yanyoendeshwa na walinda amani wa MONUSCO kutoka Tanzania.Uchambuzi mpya wa utafiti uliotolewa leo Aprili 17 na Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Wanawake, UN Women umeweka wazi kuwa zaidi ya wanawake na wasichana 38,000 wameauawa kati ya mwezi Oktoba mwaka 2023 na Desemba 2025 huko Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel ikiwa ni wastani wa takribani wanawake na wasichana 47 wanaouawa kila siku. Anold Kayanda ameufuatilia utafiti huo na kutuandalia taarifa ifuatayo.Ukatili wa kijinsia na wa kingono unatumiwa kama silaha ya vita nchini Sudan, jambo ambalo limesahaulika huku migogoro ikiendelea katika maeneo mengi mengi kote duniani amesema Tonderai Chikuhwa, Mshauri Mwandamizi wa Sera katika Ofisi ya Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Ukatili wa kijinsia katika Migogoro, katika mahojiano na Khaled Mohamed wa Idhaa ya Kiarabu ya Umoja wa Mataifa.Raia wa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, waishio mji wa Oicha uliopo Mavivi katika Jimbo la Kivu Kaskazini, wamewashukuru walinda amani kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wa Kikundi cha Tano Cha Utayari (TANZQRF-05), kinachohudumu chini ya mwamvuli wa Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda amani nchini humo (MONUSCO) kwa kutoa msaada wa dawa na huduma za kitabibu kwenye Hospitali Kuu ya Rufaa ya Mji wa Oicha wiki hii.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Hii leo jaridani tunaangazia ripoti ya mauaji wa wanawake na wasichana Gaza, ukatili wa kijinsia na wa kingono unaotumiwa kama silaha ya vita Sudan, na msaada wa dawa na matibabu ya bure nchini DRC yanyoendeshwa na walinda amani wa MONUSCO kutoka Tanzania.Uchambuzi mpya wa utafiti uliotolewa leo Aprili 17 na Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Wanawake, UN Women umeweka wazi kuwa zaidi ya wanawake na wasichana 38,000 wameauawa kati ya mwezi Oktoba mwaka 2023 na Desemba 2025 huko Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel ikiwa ni wastani wa takribani wanawake na wasichana 47 wanaouawa kila siku. Anold Kayanda ameufuatilia utafiti huo na kutuandalia taarifa ifuatayo.Ukatili wa kijinsia na wa kingono unatumiwa kama silaha ya vita nchini Sudan, jambo ambalo limesahaulika huku migogoro ikiendelea katika maeneo mengi mengi kote duniani amesema Tonderai Chikuhwa, Mshauri Mwandamizi wa Sera katika Ofisi ya Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Ukatili wa kijinsia katika Migogoro, katika mahojiano na Khaled Mohamed wa Idhaa ya Kiarabu ya Umoja wa Mataifa.Raia wa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, waishio mji wa Oicha uliopo Mavivi katika Jimbo la Kivu Kaskazini, wamewashukuru walinda amani kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wa Kikundi cha Tano Cha Utayari (TANZQRF-05), kinachohudumu chini ya mwamvuli wa Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda amani nchini humo (MONUSCO) kwa kutoa msaada wa dawa na huduma za kitabibu kwenye Hospitali Kuu ya Rufaa ya Mji wa Oicha wiki hii.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
HAKI ZA MAJIRANI

Apr 11, 2026 ·51m

Siku ya 25

Dec 24, 2021 ·6m

Siku ya 24

Dec 23, 2021 ·3m

Siku ya 23

Dec 22, 2021 ·3m

Siku ya 22

Dec 21, 2021 ·3m

Siku ya 21

Dec 20, 2021 ·3m

DANCEFLOOR MEMORIES Chahut Média DANCEFLOOR MEMORIES: Des anonymes y racontent comment, durant une nuit, le dancefloor a changé leur vie. Et comme on ne peut pas se passer de musique, on confie celle de chaque épisode à des producteurs·trices parmi les plus désirables du paysage électro mondial. Une série podcast Chahut Média réalisée en collaboration avec Motel Campo, en partenariat avec Couleur 3 & Tsugi et avec le soutien de la Ville de Genève. //Sur une idée originale de David Brun-Lambert et Carole Harari // Interviews et éditing: David Brun-Lambert // Direction musicale: Audrey Gros et Nicolas Oggier // Mix et mastering: Ismaele Gonzato // Graphic design: Ramon Valle Sapiens Bruno Carvalho Este é um podcast / audiolivro. Nele você ouvirá a leitura do livro sapiens - uma breve história da humanidade, de Yuval Noah Harari.É apenas um teste, mas espero que possa tirar algum proveito. Habari Njema za Furaha Kuu Ekklesia Africa Kila somo katika hayo masomo 25 ya kila siku, linaangazia fungu la Biblia na tafakurifupi Mwafaka kwa ajili ya usomaji wa kibinafsi na ibada za kifamilia. Masomo haya yakila siku ni njia kuu ya kutafakari uzuri wa ahadi ya wokovu kupitia kuzaliwa kwa YesuKristo. Power Of Choice Safari Afrika Tutakuangazia Duniani kote, tukikupa habari, maoni, na mitazamo mbalimbali ju ya maswala ya maisha yetu ya kila siku kama Familia, Mahusiano, Elimu, Teknolojia,Michezo, sanaa, ubunifu, mavazi na mitindo Mafanikio, lengo letu ni kuelimisha, kuburudisha na kufundisha.
URL copied to clipboard!