EPISODE · Jun 17, 2026 · 11 MIN
17 JUNI 2026
from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu · host Leah Mushi
Hii leo jaridani tunaangazia uhakika wa chakula barani Afrika, utumikishaji wa watoto jeshini Sudan Kusini, na ujumbe wa mwanaharakati wa haki za wanawake na wasichana kutoka asasi ya kiraia nchini Zimbabwe.Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la Chakula na Kilimo, FAO, pamoja na Mpango wa Chakula Duniani, WFP, yametoa onyo kali kuwa hali ya ukosefu wa uhakika wa chakula inatarajiwa kuwa mbaya zaidi kwa mamilioni ya watu katika nchi 13 zilizotajwa kuwa maeneo hatari ya njaa kati ya mwezi Juni na Novemba mwaka huu wa 2026.Watoto tisa waliokuwa wakihusishwa na vikosi vya ulinzi katika Jimbo la Equatoria Magharibi nchini Sudan Kusini wameanza safari mpya ya maisha baada ya kutambuliwa, kuachiliwa na kukabidhiwa kwa ajili ya kurejeshwa katika familia na jamii zao.Leo tunakupeleka Zimbabwe kwa mwanaharakati wa haki za wanawake na wasichana kutoka asasi ya kiraia ya “Unlimited Hope Alliance”. Kandoni mwa moja ya mikutano ya Zama Zijazo ya Umoja wa Mataifa hapa New York Marekani alipata fursa ya kuzungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii akipaza sauti kwa viongozi wa dunia kuhakikisha wanawake na wasichana wa vijijini hawapewi kisogo katika ajenda za maendeleo, elimu na teknolojia.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
What this episode covers
Hii leo jaridani tunaangazia uhakika wa chakula barani Afrika, utumikishaji wa watoto jeshini Sudan Kusini, na ujumbe wa mwanaharakati wa haki za wanawake na wasichana kutoka asasi ya kiraia nchini Zimbabwe.Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la Chakula na Kilimo, FAO, pamoja na Mpango wa Chakula Duniani, WFP, yametoa onyo kali kuwa hali ya ukosefu wa uhakika wa chakula inatarajiwa kuwa mbaya zaidi kwa mamilioni ya watu katika nchi 13 zilizotajwa kuwa maeneo hatari ya njaa kati ya mwezi Juni na Novemba mwaka huu wa 2026.Watoto tisa waliokuwa wakihusishwa na vikosi vya ulinzi katika Jimbo la Equatoria Magharibi nchini Sudan Kusini wameanza safari mpya ya maisha baada ya kutambuliwa, kuachiliwa na kukabidhiwa kwa ajili ya kurejeshwa katika familia na jamii zao.Leo tunakupeleka Zimbabwe kwa mwanaharakati wa haki za wanawake na wasichana kutoka asasi ya kiraia ya “Unlimited Hope Alliance”. Kandoni mwa moja ya mikutano ya Zama Zijazo ya Umoja wa Mataifa hapa New York Marekani alipata fursa ya kuzungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii akipaza sauti kwa viongozi wa dunia kuhakikisha wanawake na wasichana wa vijijini hawapewi kisogo katika ajenda za maendeleo, elimu na teknolojia.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
NOW PLAYING
17 JUNI 2026
No transcript for this episode yet
Similar Episodes
No similar episodes found.