EPISODE · Jun 26, 2026 · 11 MIN
26 JUNI 2026
from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu · host Feissal Kirwa
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayokupeleka jijini Nairobi nchini Kenya ambako kunafanyika Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Intaneti, IGF, mahususi kwa bara la Afrika pekee, AfIGF. Stella Vuzo, Afisa Habari wa UNIS Nairobi, Kenya amezungumza na mmoja wa vijana washiriki na kukuletea maoni yake.Idadi ya waliokufa kwenye matetemeko mawili makubwa ya ardhi yaliyokumba Venezuela wiki hii ikiongezeka na kufikia 235, afisa wa shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM nchini humo Luis Segovia akizungumza kutoka mji mkuu Caracas baada kusambaza vifaa vya dharura kwa familia amesema, “leo, IOM itaendelea kufanya kazi kwa karibu na mamlaka husika pamoja na washirika wa kibinadamu ili kuhakikisha msaada unawafikia kwa wakati wale wanaouhitaji zaidi.”Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, waambata wa wagonjwa au watu waliokufa kwa Ebola wakishindwa kusalia kwenye karantini ili kudhibiti kusambaa kwa ugonjwa huo, David Stevenson, Mwakilishi Mkazi wa shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula WFP kupitia ukurasa wa X amesema ni muhimu kuongeza usaidizi wa shirika hilo ili liweze kutoa mgao zaidi kwa wahitaji waliko, akitoa mfano wa swali alilosema rahisi lakini chungu kutoka kwa mkimbizi wa ndani Jack aliyefiwa na mwanae kwa Ebola na mkewe yuko karantini, na sasa analea watoto 13 kwa msaada wa mgao wa chakula kutoka WFP. “Kwa watoto wote hawa, mgao huu wa chakula wa mwezi mmoja utadumu kwa wiki mbili tu. Na baada ya hapo, nitawalishaje ilhali sina njia yoyote ya kufanya hivyo?”.Ripoti ya mwaka huu wa 2026 kuhusu dawa za kulevya na uhalifu imeonya kuhusu ongezeko la dawa mpya za kutengenezwa maabara huku maendeleo ya teknolojia yakiwezesha wasafirishaji kukwepa kubainika. Mkurugenzi Mtendaji wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kudhibiti Dawa za Kulevya na Uhalifu, (UNODC) Monica Juma, amesema dunia inashuhudia ongezeko ambalo halijawahi kutokea la aina mpya za dawa za kulevya, huku baadhi zikiwa na nguvu na hatari zaidi kuliko zilizokuwepo awali.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, tunasalia huko huko Nairobi Kenya kwani leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “Lengelenge lako si jipu langu”.Mwenyeji wako ni Feissal Kirwa, karibu!
What this episode covers
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayokupeleka jijini Nairobi nchini Kenya ambako kunafanyika Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Intaneti, IGF, mahususi kwa bara la Afrika pekee, AfIGF. Stella Vuzo, Afisa Habari wa UNIS Nairobi, Kenya amezungumza na mmoja wa vijana washiriki na kukuletea maoni yake.Idadi ya waliokufa kwenye matetemeko mawili makubwa ya ardhi yaliyokumba Venezuela wiki hii ikiongezeka na kufikia 235, afisa wa shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM nchini humo Luis Segovia akizungumza kutoka mji mkuu Caracas baada kusambaza vifaa vya dharura kwa familia amesema, “leo, IOM itaendelea kufanya kazi kwa karibu na mamlaka husika pamoja na washirika wa kibinadamu ili kuhakikisha msaada unawafikia kwa wakati wale wanaouhitaji zaidi.”Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, waambata wa wagonjwa au watu waliokufa kwa Ebola wakishindwa kusalia kwenye karantini ili kudhibiti kusambaa kwa ugonjwa huo, David Stevenson, Mwakilishi Mkazi wa shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula WFP kupitia ukurasa wa X amesema ni muhimu kuongeza usaidizi wa shirika hilo ili liweze kutoa mgao zaidi kwa wahitaji waliko, akitoa mfano wa swali alilosema rahisi lakini chungu kutoka kwa mkimbizi wa ndani Jack aliyefiwa na mwanae kwa Ebola na mkewe yuko karantini, na sasa analea watoto 13 kwa msaada wa mgao wa chakula kutoka WFP. “Kwa watoto wote hawa, mgao huu wa chakula wa mwezi mmoja utadumu kwa wiki mbili tu. Na baada ya hapo, nitawalishaje ilhali sina njia yoyote ya kufanya hivyo?”.Ripoti ya mwaka huu wa 2026 kuhusu dawa za kulevya na uhalifu imeonya kuhusu ongezeko la dawa mpya za kutengenezwa maabara huku maendeleo ya teknolojia yakiwezesha wasafirishaji kukwepa kubainika. Mkurugenzi Mtendaji wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kudhibiti Dawa za Kulevya na Uhalifu, (UNODC) Monica Juma, amesema dunia inashuhudia ongezeko ambalo halijawahi kutokea la aina mpya za dawa za kulevya, huku baadhi zikiwa na nguvu na hatari zaidi kuliko zilizokuwepo awali.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, tunasalia huko huko Nairobi Kenya kwani leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “Lengelenge lako si jipu langu”.Mwenyeji wako ni Feissal Kirwa, karibu!
NOW PLAYING
26 JUNI 2026
No transcript for this episode yet
Similar Episodes
No similar episodes found.