EPISODE · Jun 29, 2026 · 9 MIN
29 JUNI 2026
from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu · host Rashid Malekela
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayokupeleka mjini Caracas nchini Venezuela, mshikamano na raia wa nchi hiyo wadhihirika wakati huu wakiwa kwenye majonzi baada ya matetemeko ya ardhi kukumba wananchi. Pia tunakuletea muhtasari wa habari kama zifuatazo.Nchini Venezuela Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanaendelea kutoa msaada kufuatia matetemeko mawili ya ardhi yaliyolikumba taifa hilo wiki iliyopita. Mathalani, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP, limeripoti leo kwamba tayari limetoa zaidi ya tani elfu tatu za chakula, kiasi kinachotosha kusaidia familia zaidi ya elfu kumi kwa kipindi cha miezi miwili.”Huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia Congo DRC, raia wameelezea haki zao zinazokiukwa ikiwemo kuzuiwa kupatiwa misaada ukatili wa kingono na mauaji. Maelezo hayo yamo kwenye ripoti iliyotolewa leo na Tume Huru ya Umoja wa Mataifa inayochunguza hali ya haki za binadamu katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini, ikiwa ni ripoti yao ya kwanza mbele ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mjini Geneva, Uswisi?”.Na, michuano ya Fainali ya Kombe la Dunia la Mpira wa Miguu inaendelea huku dunia ikishuhudia ongezeko la joto kali. Katika juhudi za kulinda wachezaji, wafanyakazi na mashabiki dhidi ya athari za joto, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO, Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema “WHO tunashirikiana na FIFA na nchi zinazoandaa michuano hiyo katika kampeni iitwayo Beat the Heat inayolenga kuweka mipango ya utekelezaji, kutoa elimu kwa wananchi, kuanzisha mifumo ya tahadhari za mapema, kuboresha upatikanaji wa maji salama ya kunywa, pamoja na kuweka maeneo ya kujipooza.”Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
What this episode covers
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayokupeleka mjini Caracas nchini Venezuela, mshikamano na raia wa nchi hiyo wadhihirika wakati huu wakiwa kwenye majonzi baada ya matetemeko ya ardhi kukumba wananchi. Pia tunakuletea muhtasari wa habari kama zifuatazo.Nchini Venezuela Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanaendelea kutoa msaada kufuatia matetemeko mawili ya ardhi yaliyolikumba taifa hilo wiki iliyopita. Mathalani, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP, limeripoti leo kwamba tayari limetoa zaidi ya tani elfu tatu za chakula, kiasi kinachotosha kusaidia familia zaidi ya elfu kumi kwa kipindi cha miezi miwili.”Huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia Congo DRC, raia wameelezea haki zao zinazokiukwa ikiwemo kuzuiwa kupatiwa misaada ukatili wa kingono na mauaji. Maelezo hayo yamo kwenye ripoti iliyotolewa leo na Tume Huru ya Umoja wa Mataifa inayochunguza hali ya haki za binadamu katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini, ikiwa ni ripoti yao ya kwanza mbele ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mjini Geneva, Uswisi?”.Na, michuano ya Fainali ya Kombe la Dunia la Mpira wa Miguu inaendelea huku dunia ikishuhudia ongezeko la joto kali. Katika juhudi za kulinda wachezaji, wafanyakazi na mashabiki dhidi ya athari za joto, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO, Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema “WHO tunashirikiana na FIFA na nchi zinazoandaa michuano hiyo katika kampeni iitwayo Beat the Heat inayolenga kuweka mipango ya utekelezaji, kutoa elimu kwa wananchi, kuanzisha mifumo ya tahadhari za mapema, kuboresha upatikanaji wa maji salama ya kunywa, pamoja na kuweka maeneo ya kujipooza.”Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
NOW PLAYING
29 JUNI 2026
No transcript for this episode yet
Similar Episodes
No similar episodes found.