EPISODE · Mar 24, 2026 · 1 MIN
JIFUNZE KISWAHILI: METHALI
from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu · host RASHID MALEKELA/JOSEPHAT GITONGA
Hii leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “Ateteaye mtuku ni tanguko la bure."Dkt. Gitonga anasema, "Mtuku ni mtu asiyefaa au asiyeweza kutegemeeka. Methali hii ina maana kwamba mtu asiyetegemeeka kamwe katika jamii na ambaye hana utu, kumtetea ni kujidhalilisha wewe mwenyewe. Ni kazi bure isiyo na faida. Ukimtetea apate labda cheo au kazi fulani utajilaumu mwenyewe kwani hatawajibika hata kamwe. Inatuelimisha kwamba iwapo utakuwa radhi kumtetea mtuku basi kuwa tayari kuhusishwa naye. Tetea walio wema si waovu."
What this episode covers
Hii leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “Ateteaye mtuku ni tanguko la bure."Dkt. Gitonga anasema, "Mtuku ni mtu asiyefaa au asiyeweza kutegemeeka. Methali hii ina maana kwamba mtu asiyetegemeeka kamwe katika jamii na ambaye hana utu, kumtetea ni kujidhalilisha wewe mwenyewe. Ni kazi bure isiyo na faida. Ukimtetea apate labda cheo au kazi fulani utajilaumu mwenyewe kwani hatawajibika hata kamwe. Inatuelimisha kwamba iwapo utakuwa radhi kumtetea mtuku basi kuwa tayari kuhusishwa naye. Tetea walio wema si waovu."
NOW PLAYING
JIFUNZE KISWAHILI: METHALI
No transcript for this episode yet
Similar Episodes
No similar episodes found.