EPISODE · Aug 6, 2026 · 9 MIN
06 AGOSTI 2026
from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu · host Flora Nducha/ Feissal Kirwa
Leo tunaangazia hatua kubwa katika mapambano dhidi ya Virusi Vya Ukimwi, VVU, ambapo Zimbabwe imekuwa miongoni mwa nchi za kwanza duniani kuanza kutoa Lenacapavir, sindano ya kinga inayotolewa mara mbili tu kwa mwaka na yenye ufanisi wa zaidi ya asilimia 96 katika kuzuia maambukizi mapya ya VVU. Hatua hiyo inaimarisha juhudi za nchi hiyo yenye kiwango cha maambukizi cha asilimia 11.2, ikilenga zaidimakundi yaliyo hatarini, hususan wasichana balehe na wanawake vijana ambao wanaendelea kubeba mzigo mkubwa wa maambukizi. Hata hivyo, pamoja na matumaini hayo, changamoto za upatikanaji wa dawa hiyo, gharama, unyanyapaa pamoja na ufikiaji wa huduma katika maeneo ya vijijini bado zinaendelea kuathiri kasi ya mafanikio. Kupitia video iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na UKIMWI, UNAIDS, Feissal Kirwa wa idhaa hii amefuatilia kwa kina.
Embed this episode
NOW PLAYING
06 AGOSTI 2026
No transcript for this episode yet
Similar Episodes
No similar episodes found.
Similar Podcasts
No similar podcasts found.