EPISODE · Jul 16, 2026 · 9 MIN
16 JULAI 2026
from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu · host Feissal Kirwa
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka Ukanda wa Gaza ambako sitisho la mapigano kati ya Israeli na Palestina lililotiwa Saini tarehe 10 mwezi Oktoba mwaka jana wa 2025 limewezesha wakulima wa eneo hilo kurejea mashambani. Pia tunakuletea Muhtasariw a habari.Mashirika mawili ya Umoja Umoja wa Mataifa lile la Uhamiaji, IOM na la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR kupitia taarifa waliyoitoa kwa pamoja jijini Gneva Uswusi na BangKok Thailand, wameeleza wasiwasi mkubwa kufuatia taarifa kwamba boti mbili zilizokuwa zimebeba zaidi ya watu 500 huenda zimezama katika pwani ya Myanmar katika siku za hivi karibuni. Kwa mujibu wa taarifa za awali, boti hizo mbili ziliondoka mwishoni mwa mwezi Juni kutoka Jimbo la Rakhine nchini Myanmar zikiwa zimewabeba zaidi ya abiria wa jamii ya Rohingya, wakiwemo baadhi waliokuwa wametoka katika kambi za wakimbizi za Cox's Bazar nchini Bangladesh.Zaidi ya watoto milioni 23 wengine zaidi ya wale ambao wako tayari kwenye umaskini duniani wanaweza kutumbukia katika umaskini wa kipato ifikapo mwisho wa mwaka huu wa 2025 kutokana na kuendelea kwa mzozo wa Mashariki ya Kati na athari zake kwa biashara ya kimataifa, kwa mujibu wa ripoti mpya iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) jijini New York, Marekani.Na Uganda leo imeanza rasmi kuhesabu siku 42 kuelekea kutangazwa kumalizika kwa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola baada ya mgonjwa wa mwisho aliyethibitishwa kuwa na maambukizi kupimwa mara ya pili na kubainika hana virusi hivyo, kisha kuruhusiwa kutoka hospitalini. Hatua hiyo ni mafanikio muhimu katika juhudi za nchi hiyo kudhibiti mlipuko, imesema taarifa iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, WHO ofisi ya Uganda.Mwenyeji wako ni Feissal, karibu!
What this episode covers
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka Ukanda wa Gaza ambako sitisho la mapigano kati ya Israeli na Palestina lililotiwa Saini tarehe 10 mwezi Oktoba mwaka jana wa 2025 limewezesha wakulima wa eneo hilo kurejea mashambani. Pia tunakuletea Muhtasariw a habari.Mashirika mawili ya Umoja Umoja wa Mataifa lile la Uhamiaji, IOM na la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR kupitia taarifa waliyoitoa kwa pamoja jijini Gneva Uswusi na BangKok Thailand, wameeleza wasiwasi mkubwa kufuatia taarifa kwamba boti mbili zilizokuwa zimebeba zaidi ya watu 500 huenda zimezama katika pwani ya Myanmar katika siku za hivi karibuni. Kwa mujibu wa taarifa za awali, boti hizo mbili ziliondoka mwishoni mwa mwezi Juni kutoka Jimbo la Rakhine nchini Myanmar zikiwa zimewabeba zaidi ya abiria wa jamii ya Rohingya, wakiwemo baadhi waliokuwa wametoka katika kambi za wakimbizi za Cox's Bazar nchini Bangladesh.Zaidi ya watoto milioni 23 wengine zaidi ya wale ambao wako tayari kwenye umaskini duniani wanaweza kutumbukia katika umaskini wa kipato ifikapo mwisho wa mwaka huu wa 2025 kutokana na kuendelea kwa mzozo wa Mashariki ya Kati na athari zake kwa biashara ya kimataifa, kwa mujibu wa ripoti mpya iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) jijini New York, Marekani.Na Uganda leo imeanza rasmi kuhesabu siku 42 kuelekea kutangazwa kumalizika kwa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola baada ya mgonjwa wa mwisho aliyethibitishwa kuwa na maambukizi kupimwa mara ya pili na kubainika hana virusi hivyo, kisha kuruhusiwa kutoka hospitalini. Hatua hiyo ni mafanikio muhimu katika juhudi za nchi hiyo kudhibiti mlipuko, imesema taarifa iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, WHO ofisi ya Uganda.Mwenyeji wako ni Feissal, karibu!
NOW PLAYING
16 JULAI 2026
No transcript for this episode yet
Similar Episodes
No similar episodes found.