FAO yawezesha wanawake na vijana katika sekta ya mwani Zanzibar episode artwork

EPISODE · Aug 17, 2026 · 2 MIN

FAO yawezesha wanawake na vijana katika sekta ya mwani Zanzibar

from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu · host Leah Mushi / Assumpta Massoi

Nchini Tanzania hususan visiwani Zanzibar, Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, (FAO) tangu mwaka 2019, kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wanaimarisha sekta ya mwani, kwa kuwekeza katika mafunzo yanayolenga kuongeza uzalishaji, tija na kipato. Miongoni mwa walionufaika zaidi ni vikundi vya wanawake, ambavyo vimejengewa uwezo kuhusu mbinu bora za uzalishaji, uanikaji na uhifadhi wa mwani, pamoja na kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi. Assumpta Massoi anatuletea taarifa inayomhusu mnufaika mmoja wa mafunzo hayo.(Taarifa ya Assumpta Massoi)Jumla ya vikundi 33 vya wanawake vimewezeshwa kwa chanja bora za kuanikia mwani na maturubai maalum ya kuufunika wakati wa mvua.Aidha, wanawake wamejengewa uwezo kuhusu teknolojia ya kilimo mchanganyiko inayowawezesha kulima mwani sambamba na kufuga majongoo bahari.Teknolojia hii inalenga kuongeza tija, kuboresha matumizi ya rasilimali za bahari na kuwawezesha wanawake kupata vyanzo mbalimbali vya kipato.FAO pia imewawezesha vijana kupitia Zanzibar Technology and Business Incubator (ZTBI), kwa kuwapatia mafunzo kuhusu usindikaji, ubunifu na uongezaji thamani wa bidhaa za mwani. Mafunzo hayo yamejikita pia katika uboreshaji wa ubora, upatikanaji wa ithibati na masoko, huku vijana wakipatiwa vifaa vya kuendeleza uzalishaji na ujasiriamali katika sekta ya mwani.

Episode metadata supplied by the publisher feed · Published Aug 17, 2026

Embed this episode

NOW PLAYING

FAO yawezesha wanawake na vijana katika sekta ya mwani Zanzibar

0:00 2:22

No transcript for this episode yet

We transcribe on demand. Request one and we'll notify you when it's ready — usually under 10 minutes.

No similar episodes found.

No similar podcasts found.

Frequently Asked Questions

How long is this episode of Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu?

This episode is 2 minutes long.

When was this Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu episode published?

This episode was published on August 17, 2026.

Can I download this Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu episode?

Yes. Use the download control on the episode player to save the publisher-provided media file.
URL copied to clipboard!